Picha: Basi la abiria lateketea kwa moto vituo 4 kabla ya kuingia Ubungo, Dar

Basi lenye namba za usajili T990 AQF la kampuni ya Safari Njema liililokuwa likitokea Dodoma kuja jijini Dar, limeteketea kwa Moto maeneo ya Kimara Stop Over-Suka,mara baada ya kugongana na Lori lililokuwa limebeba shehena ya mifuko ya Cement (namba zake za usajili hazikujulikana mara moja),jioni ya leo,Inaelezwa kuwa mali zote zilikowemo katika basi vimeteketea kabisa kwa moto,hali ya abiria waliokuwemo ndani ya basi hilo tutawaleta taarifa kamili itakayotolewa na Jeshi la Polisi.
Pichani Lori kama lionekavyo likiwa nyuma ya basi baada ya kugongana kusababisha mlipuko mkubwa wa moto na kupelekea magari yote mawili kuwaka moto .
 Baadhi ya mashuhuda wakishuhudia tukio hilo lilivyokuwa
 Gari la zima moto likiwa eneo la tukio kuuzima moto huo.







Baadhi ya Vijana wasio waaminifu walivamia eneo hilo la ajali na kuanza kuondoka na mifuko ya Cement iliyokuwa imebebwa na Lori hilo.


Post a Comment

0 Comments