NEWSPicha,Mwanafunzi aliyepondwa na mwalimu baada ya kuvaa vazi la kiafrika kwenye sherehe nchini Marekani


Binti aliyevaa nguo ya kiafrika kwenye sherehe za Pron kwenye shule yao nchini Marekani amelalamika kwa kupondwa na mwalimu kuwa nguo yake haijaendana na shughuli yenyewe.

Dada anayefahamika kama Mayalaya Zanders ,amevaa nguo ya mtindo wa Ankara ambayo ni maarufu nje na ndani ya Afrika ila mwalimu wake aliona kama kakosea kitu ambacho kilimkera dada huyu.

Mayalaya Zanders ana miaka 17 na anasoma shule ya sekondari ya Garfield Heights High School huko Cleveland, Ohio, alimwambia mwalimu wake juu ya muonekano na nguo yake kuwa tofauti na wanafunzi wote kwenye pati hio ila mwalimu alimwambia anaonekana kuwa “tacky for prom.”




Post a Comment

0 Comments